Burudani

Huu ndio ulikuwa ujumbe wa Jux kwa Vanessa kwenye Valentine’s Day

Japo Vanessa Mdee amekuwa katika wakati mgumu baada ya jina lake kutajwa kwenye orodha ya mkuu wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya majina ya watu wanaodaiwa kuhusika kwenye madawa ya kulevya lakini mpenzi wake Jux ameonyesha kuziba masikio na kumjali zaidi.

Hitmaker huyo wa Wivu, kupitia mtandao wa Instagram, Jumanne hii ikiwa ni siku ya wapendanao (Valentine’s Day) amemuandikia ujumbe Vanessa ambao unaonyesha kuwa amemteka zaidi katika himaya yake ya mapenzi. Kupitia mtandao huo, Jux ameandika, “❤️ #happyvalentinesday#umenikamata.”

Wapenzi hao pia wameshirikiana kwenye wimbo wa ‘Juu’ ambao mpaka sasa umeshatazamwa kwa mara 1,160,942 kwenye mtandao wa Youtube.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents