Burudani
Hussein Machozi kuachia video ya wimbo mpya ‘Manyoni Si Mbali’ mwezi ujao
Ni nyimbo nyingi za bongo zilizotoka tangia mwaka huu uanze, na bado wasanii wengine wameahidi kutoa kazi zao mpya hivi karibuni akiwemo Hussein Machozi, anayetarajia kuachia single mpya iitwayo ‘Manyoni Si Mbali’.
Hussein ameiambia Bongo5 kuwa video ndio itatangulia kutoka mwezi ujao (July 5) na kufuatiwa na audio.
Machozi ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya ni msanii kutoka Manyoni, Singida hivyo katika wimbo huu ameamua kupagusia nyumbani kidogo.
Audio na video vyote vimefanyika nchini Kenya. Video imesimamiwa na director anaezidi kupata umaarufu bongo Enos Olik aliyefanya video ya Weusi ‘Gere’, na ya Jaguar ‘Kioo’.