Habari
Hussein Machozi afanya collabo na kundi la Sauti Sol la Kenya
Hit maker wa ‘Addicted’ Hussein Rashid maarufu kama Hussein Machozi ambaye amekuwa nchini Kenya siku za hivi karibuni amefanya collabo na mastaa wa kundi la Sauti Sol.
Hivi Karibuni Hussein aliweka picha akiwa na moja wa members wa kundi hilo aitwaye Baraza wakiwa studio, na baadaye Sauti Sol wamethibitisha juu ya collabo hiyo kupitia twitter.
Hussein Machozi on Churchill. Yes – it's true we have done a song together. Hope you will all love it when it's out.
— Sauti Sol (@SautiSol) September 15, 2013
Saut Sol ni kundi lenye mafanikio makubwa kimataifa ambalo mwaka jana lilishinda Channel O VMA kupitia collabo yao na AY ‘I don’t wanna be alone’, na mwaka huu pia wamefanikiwa kuingia katika tuzo hizo na wimbo wao ‘Money Lover’.