Burudani

Hussein Machozi adai kuwa nafasi yake kwenye muziki bado ipo

Msanii wa Bongo Fleva, Hussein Machozi amesema kuwa muziki wa sasa unaofanyika ni wa kiki lakini atafanya vizuri kwa sababu nafasi yake kwenye muziki bado ipo kwa kuwa hakuna aliyefanya kama yeye mpaka sasa.

hussein_machozi

Akiongea na Bongo5, Hussein Machozi amesema kuwa nafasi yake kwenye muziki bado ipo kwa sababu hakuna aliyefanya kama yeye mpaka sasa.

“Game ni rahisi sana, kwa sababu muziki wa sasa hivi ni kiki. Mimi nitafanya muziki lakini kama ukinambia nifanye kiki nitashindwa,” alisema Machozi.

“Siyo kama nitarudisha heshima mimi nina heshima mpaka kesho kwa sababu hakuna mtu aliyeweza kufanya kama mimi. Najiamini najua nafasi yangu bado ipo sema nilikuwa kimya kidogo,” aliongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents