Burudani

Hizi ni nchi za Afrika zinazoongoza kuwa na wanawake wazuri?

Afrika ni miongoni mwa mabara saba duniani yenye wanawake wazuri na wenye mvuto.

140616Messi-jpg

Uzuri wa wanawake wengi kutoka bara la Afrika unatokana na rangi zao nyeusi za asili, japo wapo wengi wanatumia vipodozi ili kujichubua ili wapate rangi nyeupe na baadaye madawa hayo huwaletea madhara kwenye miili yao.

Hizi ni nchi za Afrika zenye wanawake wazuri zaidi?

5. Angola

140616Messi-jpg

Nchi ya Angola ni kama Brazil ya Afrika, hili linakuja kutokana na uzuri walionao wanawake kutoka Angola kufanana zaidi na wale wa Brazil. Wanawake wa Angola wamebarikiwa kuwa na maumbo makubwa yaliyojengeka kama wabrazil lakini tofauti yao wakiwa asilimia 100 rangi ya ngozi zao ni halisia huku wale wa Brazil wengi wakiwa wanaongoza kwa kufanya plastic surgery.

4. Cape Verde Island

11419262_1157084614313211_1074544956_n

Viwango vya Fifa vilivyotoka mwaka huu, vinaonyesha kuwa nchi ya Cape Verde inaongoza kwa Afrika. Hilo halijaishia hapo pia nchi ya Cape Verde imebarikiwa kuwa na wanawake wazuri.

Raia wa nchi hiyo wana mchanganyiko wa bara la Ulaya na Afrika kwa pamoja, ukikutana na mwanamke kutoka Cape Verde hutoacha kugeuka na kumuangalia muda wote kutokana na uzuri alio nao pamoja na urefu waliobarikiwa kama twiga anapokuwa mbugani.

3. Ethiopia

140616Messi-jpg

Ethiopia ni nchi ambayo ni nyumba ya wanawake wazuri Afrika. Wapo waliosema mchanganyiko walionao Yemen na Ethiopia ndiyo unawafanya wanawake wa nchi hiyo kuwa wazuri na wenye mvuto zaidi. Tabasamu la wanawake wa Ethiopia linamvutia hata asiyekuwa na njaa akikaribishwa kula lazima ataenda.

2. Somalia

11419262_1157084614313211_1074544956_n

Moja kati ya nchi zenye madhara makubwa ya vita ni nchi ya Somalia. Tangu vita ianze mwaka 1992 mpaka leo Somalia imekuwa ni nchi kame sana.

Japo kumekuwepo kwa vita kwa muda wote huo lakini Somalia ni miongoni mwa nchi zilizobarikiwa kuwa na wanawake wazuri kwenye bara la Afrika. Rangi yao zao za chocolate na ujasiri wao unawafanya wawe ni miongoni mwa wanawake wazuri. Vita haiwezi kuharibu uzuri wa wanawake wa Somalia.

1. Rwanda

11419262_1157084614313211_1074544956_n

Nchi ya Rwanda ni miongoni mwa nchi zenye wanawake wazuri Afrika. Rangi yao na maumbo yao yameweza kuyavutia wanaume kibao kutamani kuwa na mwanamke wa Rwanda. Ukimuona Ange Kagame utaweza ni malaika, lakini ukweli unabaki kuwa anatoka Rwanda.

Japo wapo wachache kwenye taifa lao na uzuri wao bado wameonekana kuwa ni wapambanaji wasioweza kukata tamaa kwa haraka. Wanawake wa Rwanda ni kama mapple ya peponi yaliyopo Afrika.

Nchi zingine zenye wanawake wazuri kwa Afrika ni pamoja na; Afrika Kusini, Nigeria, Ghana, Kenya na Tanzania.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents