Hizi ni chati za Afrika ambazo ‘Never Ever’ ya Vanessa Mdee inasumbua kwa sasa
Wimbo wa Vanessa Mdee ‘Never Ever’ ambao video yake ilianza kutoka October 9 kwa kutambulishwa kupitia Trace Urban na kufatiwa na audio iliyotoka Oct 12, unaendelea kushika chati mbalimbali za vituo vya TV pamoja na radio barani Afrika.
Baadhi ya chati ambazo wimbo huo uliopikwa na producer anayesumbua sana kwa sasa Nahreel wa The Industry na video kuongozwa na Justin Campos, ni pamoja na Africa Top 10 ya Trace Urban ambapo kwa wiki hii imekamata nafasi ya pili.
Chati nyingine ni Africa Top 10 ya Nigezie TV ya Nigeria ambapo iko nafasi ya tatu.
NO 3. @VanessaMdee – NEVER EVER #AfricaTop10
— Nigezie Tv (@NigezieTV) November 27, 2015
‘Never Ever’ pia iko nafasi ya nne kwenye chati ya kituo cha radio cha Afrika Kusini, YFM
No 4: Repping #Tanzania @VanessaMdee – Never Ever #AfricaBoomBoxx pic.twitter.com/XCzWdovqTt
— #Yfm (@Yfm) November 27, 2015
Kwenye chati ya NAIJA 102.7 FM IB ya Nigeria iko namba moja.
#NP NEVER EVER @VanessaMdee
Ontop #SatodayEveningJollof #AfricanTopTen No1
with @georgewisdom3
— NAIJA 102.7 FM IB (@NAIJA102IBADAN) November 21, 2015
Kwenye African Count Down ya Crooze Fm ya Uganda iko nafasi ya nne
#4. @VanessaMdee – Never Ever (up 1)
#AfricanCountdown
— WesternUg'zBiggest (@912CroozeFM) November 26, 2015
Kwenye African Top 10 ya The Beat Fm ya Nigeria iko nafasi ya kwanza
#AfricanTop10 on the #MorningRushIB w/ @WaleOzolua & @JosieAmiegbe
No.01: Never Ever – @VanessaMdee
— THE BEAT 97.9 FM (@THEBEAT979FM) November 25, 2015