Bongo Movie
Hemed Akatazwa kuigiza na mama yake
Mwanamuziki wa kizazi kipya na mwigizaji katika filamu Hemedi, amesema anamalizia mkataba wake wa mwisho na filamu na kuachana nayo kabisa kazi hiyo ya uigizaji, kutokana na mama yake kutopendezewa na sanaa hiyo.
Akizungumizia suala hilo, alisema mama yake amekuwa hapendezwi kabisa na kazi hiyo ya sanaa kutokana na mavazi wanayovaa na jinsi anavyoshikana na wanawake bila stala yoyote. Hemed Amesema ameamua kuachana kabisa bila ya pingamaizi kwani hata hivyo haimlipi wala hamisaidii katika maisha yake zaidi ya kufanya kama ‘Hobe’.
Anasema zaidi ya kuacha kazi ya filamu atapata muda muafaka wa kufanya kazi yake ya muziki, ambayo amekuwa akimisi kwa muda mrefu, hata hivyo amedai kwamba anamalizia mikataba aliyokuwa ameshasaini.