Elizabeth ‘Lulu’ Michael, ni shabiki mkubwa wa muziki.
Wiki iliyopita, muigizaji huyo alihost show ya Ngaz Kwa Ngaz ya EATV na kucheza video za nyimbo 20 za mwaka jana anazozikubali. Alikuwa na maoni mbalimbali kuhusu nyimbo hizo.
Kuhusu Dume Suruali wa Mwana FA f/ Vanessa Mdee
Alisema Vanessa Mdee alikuwa mtu sahihi kushirikishwa kwenye Dume Suruali
Alisema kama video ya Dume Suruali ingefanyika kwenye mazingira ya Tanzania ingepata story nyingi na ingekuwa bora
Kuhusu Moyo Mashine wa Ben Pol
Alisema alishangaa kubaini kuwa Moyo Mashine uliandikwa na muimbaji wa gospel Godluck Gosbert
Alisema video ya Moyo Mashine hajawahi kuielewa
‘Ben Pol ni mmoja wapo wa wasanii ambao inabidi tujivunie’
Kuhusu Perfect Combo wa Joh Makini f/ Chidinma
Alisema anampenda Chidinma na watu husema kuna namna wanafanana
Alidai Joh Makini na Chidinma wameingiza msemo mpya mjini ‘Perfect Combo’
Kuhusu Lover Boy wa Barnaba
Alisema hakufikiria kama video ya wimbo Lover Boy ilifanyika Bongo
‘ Dread za Barnaba zimekuwa vizuri, smart zimekuwa ndefu zinavutia zaidi kuliko mwanzo zilikuwa kama misumari’
Alimmwagia sifa model kwenye video ya Lover Boy, anasema ametulia sana na amevaa vizuri
Kuhusu Sweet Mangi wa Nick wa Pili
Alisema alikuwa anajiuliza ni vipi Nick wa Pili alifahamu aina za nywele alizozitaja kwenye wimbo
Alidai G-Nako ameifanya video ya Sweety Mangi aipende zaidi
Kuhusu Kokoro wa Rich Mavoko f/ Diamond
Alimuelezea Mavoko kama msanii mwenye kipaji cha aina yake
Alisema alikuwa model kwenye video ya kwanza ya Mavoko ambaye anasema alikuwa anamuogopa hata kumshika Lulu
Alikiri kuwa video ya Kokoro haijambariki
Kuhusu Kajiandae wa Ommy Dimpoz na Alikiba
‘Ommy Dimpoz akikaa na Alikiba wana chemistry fulani hivi lazima wafanye kitu kizuri’
Aliwapongeza Ommy na Kiba kwa kuipa video mazingira ya Kiafrika zaidi
Kuhusu Muziki wa Darassa
Alisema Muziki ya Darassa umefanya vizuri bila hata kutumika nguvu nyingi
Alisema Muziki ni wimbo anaoupenda sana mama yake
Alimuelezea Darassa kama msanii mnyenyekevu asiyejisikia