Habari

Hawa ndio mastaa waliompatia Harmorapa jina hilo

Harmorapa amefunguka kwa kuwataja mastaa waliosababisha kutumia jina analotumia sasa kwenye muziki.

Akingea kwenye kipindi cha Bongo Dot Home cha Times FM, rapper huyo amemtaja Roma na Mr T-Touch kuwa ni watu ambao walimshauri kutumia jina la Harmorapa.

“Baadhi ya mastaa wakubwa katika muziki wa hapa Bongo nao walinishauri nijiite hivi, akiwemo brother Roma Mkatoliki na Mt T-Touch,” amesema rapper huyo.

Harmo ameongeza kuwa kabla ya kutumia jina hilo alikuwa akifahamika kwa jina la Jembe la Kusini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents