Hasheem Thabeet, Diamond na Wema Sepetu wanaongoza kwa kuwa na followers wengi Instagram
Baada ya Facebook na Twitter, Instagram ni mtandao wa kijamii nchini Tanzania wenye watumiaji wengi zaidi. Watu wengi huipenda Instagram kutokana na uwezo wake wa kupendezesha picha na kuwa na muonekano wa kuvutia zaidi.
Kama Instagram ingekuwa inapatikana kwenye simu za Blackberry, bila shaka mpaka sasa ungekuwa na watumiaji idadi sawa na waliopo kwenye Twitter.
Instagram ni mtandao unaopendwa zaidi na mastaa wa Tanzania ambapo unaweza kuwapata wengi zaidi huko kuliko Facebook ama Twitter. Hawa ndio mastaa wa Tanzania wenye followers wengi zaidi. Idadi hii ni kwa mujibu wa siku ya leo June 19.
Hasheem Thabeet
36,227
Diamond Platnumz
29,330
Wema Sepetu
13,352
Jokate Mwegelo
8,909
Elizabeth Michael Lulu
8,870
Vanessa Mdee
8,278
Flaviana Matata
7,683
Nancy Sumari
7,374