Burudani
Hapa Kazi Tu: Said Fella achimba visima vilivyokwama kwa miaka mitatu kwenye kata ya Kilungule (Picha)
Kasi ya Rais Dkt John Magufuli ya kupiga kazi tu imewaambukiza viongozi wengi.
Muasisi wa Mkubwa na Wanawe, Said Fella ambaye pia ni diwani wa kata ya Kilungule ya wilayani Temeke, Dar es Salaam ameanza kutekeleza ahadi zake.
Fella ameiambia Bongo5 kuwa ameanza kwa kuvirejesha visima vilivyokuwa vimeshindwa kutoa maji kwa miaka mitano iliyopita. Chini ni picha za kazi hiyo.
Amesema wakati wa kampeni aliahidi kuwa angeanza kushughulikia kero ya maji kwenye kata yake ndani ya siku 30. Ameongeza pamoja na visima, aliahidi pia kujenga kituo cha polisi kwenye kata hiyo pamoja na kutengeneza barabara.