Burudani

Goodluck Gozbert (Lollipop) autaja wimbo wa Bongo Fleva alioukubali 2016

Muimbaji wa muziki wa injili nchini Goodluck Gozbert ameutaja wimbo wa Bongo Fleva alioukubali kwa mwaka jana.

Hitmaker huyo wa Acha Waambiane, ameutaja wimbo wa ‘Muziki’ wa Darassa ndio wimbo wake bora kwa mwaka jana kwa kuwa amekuwa akiusikia sana ukipigwa sehemu mbalimbali.

“Wimbo wa Darassa nimekuwa nikiusikia sana ukipigwa kuliko kuusikiliza, so far nikaamua kutulia na kusikia kilichoimbwa nikatokea kuupenda,” Goodluck amekiambia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM Jumatano hii.

Mpaka sasa wimbo huo umeshatengeneza CV kubwa kwa rapper Darassa huku ukiwa umetazamwa mara milioni 2.8 kwenye mtandao wa YouTube tangu ulipotoka mwezi Novemba mwaka jana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents