Burudani
Good Timing? Ali Kiba aonjesha kava la single yake mpya
Ali Kiba anakuja tena!!! Baada ya kusubiriwa kwa takriban miaka miwili, hitmaker huyo wa ‘Dushelele’, anatarajia kuachia ngoma mpya siku chache zijazo. Picha za kava linaloonekana kuwa ni la ngoma yake hiyo zimeenza kuonekana Jumatatu hii kwenye mtandao wa Instagram.
Ali Kiba ataachia ngoma hiyo katika kipindi ambacho amemake headlines kutokana na kauli iliyomlenga Diamond akisema kuwa hajachukua nafasi yake. Diamond amejibu kauli hiyo kupitia Instagram.