Habari

Gharama kubwa kukwamishwa uchaguzi wa Rais, Congo

Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imesema haitoweza kumudu gharama za uchaguzi wa Rais uliokuwa umepangwa kufanyika mwaka huu, serikali imesema.

Waziri wa bajeti, Pierre Kangudia amesema gharama za kuendesha uchaguzi ambazo ni dola bilioni 1.8 ni kubwa mno. Mwaka jana, serikali na upinzani vilikubaliana kufanya uchaguzi mpya mwishoni mwa mwaka huu.

Utawala wa Rais Joseph Kabila ulimalizika November 2016. Wapinzani wa Kabila wamemshutumu kwa kuendelea kuchelewesha uchaguzi ili aendelee kukaa madarakani.

Kabila aliingia madarakani mwaka 2001 baada ya kuuawa baba yake, Laurent Kabila.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents