Burudani
Galaxy: Sipo tayari kufanya kazi na directors wa bongo kwa sasa
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Galaxy, ambaye kwa sasa wimbo wake wa ‘Mzuri tu’ bado unafanya vizuri tangu ameuachia japo kuwa bado hajaachia video yake, amesema hana plan ya kufanya kazi na directors wa bongo kwa sasa.
Galaxy ambaye kwa sasa anakaribia kusafiri kuelekea nchini Kenya kufanya video mbili ikiwemo moja ya Mzuri tu na moja kati ya madirector wakubwa wa nchini humo ameiambia Bongo5:
“Kuanzia next week ninaweza nikasafiri kuelekea nchini Kenya kushoot video mbili za nyimbo zangu moja ikiwa ya Mzuri tu. Nimeamua kufanya hivyo sababu nimefanya research na nimeona kuwa directors wa hapa bongo bado hawana kitu ambacho nakitaka kwenye video zangu zinazokuja na nataka kufanya video kubwa kuliko ile ya Tam Tam.”