Burudani
Fundi Samweli kutayarisha wimbo wa Marco Chali, ni sehemu ya mradi wake kama msanii
Producer wa Sweden, Fundi Samweli, atatayarisha wimbo mpya wa producer wa MJ Records, Marco Chali.
Fundi Samwel akiwa na Marco Chali kwenye studio za MJ Records
Marco ameaimbia Bongo5 kuwa Fundi Samweli ni mtayarishaji wa muziki anayemkubali na anaupenda muziki na hivyo kufanya naye kazi itakuwa ni kitu kizuri kwake. Amesema wamezungumza na producer huyo kuwa atamtengenezea beat ambayo Marco ataiandikia na kurekodi sauti kwenye studio ya MJ ambazo atamtumia Sweden ili azioanishe na beat yake na kukamilisha kila kitu.
Marco amesema wimbo atakaofanya na Fundi Samwel utakuwa sehemu ya mradi anaoufanya yeye kama msanii na maproducer wengine wakubwa wa Tanzania na kwamba yeye hatoshiriki katika kutayarisha chochote.