Burudani
Frank Ocean abadili jina lake kisheria
Frank Ocean amelifanya jina hilo kuwa lake kisheria.
Kwa mujibu wa TMZ, Ocean amebadili jina lake kutoka Christopher Edwin Breaux ambalo ndilo alilozaliwa nalo na sasa atajulikana kwa jina la muziki, Frank Ocean.
Ocean alikuwa abadili jina lake tangu mwaka jana lakini jaji wa Los Angeles alichelewesha mchakato hadi pale aliposhughulikia kusitishwa kwa leseni yake ya udereva.
Muimbaji huyo mwenye miaka 27 anatarajia kuachia album yake, Boys Don’t Cry July mwaka huu.