Bongo Movie

Flora Mvungi amkingia kifua H.Baba dhidi ya madai ya Irene Uwoya


Baada ya mrembo na muigizaji wa filamu nchini Tanzania,Irene Uwoya kuliambia gazeti la Baabkubwa kuwa katika wanaume ambao hawezi kurudiana nao, H.Baba ni wa kwanza kwasababu ni ‘mchovu’ kitandani, mpenzi wake mpya Flora Mvungi ameibuka kujibu shutuma hizo.
Kupitia Clouds Fm jana, Flora amesema anamshangaa Irene kwa madai hayo, na kusema kuwa H.Baba humpagawisha kwa an ‘earth shaking and mind-blowing sex’ na huenda yeye (Irene) alikuwa anadate na H.Baba mwingine.
Flora amesema katika uhusiano wote na msanii huyo wa Bongo Flava amekuwa akiridhishwa na wala haoni hayo anayoyasema Irene.
Ameongeza kuwa anachojua yeye ni kuwa mapenzi ni kusikilizana na kuzungumza,kuheshiamiana,kujaliana na mwisho kabisa suala la kitandani ndio hufuata ambalo hata hivyo mzee wa ‘Mpenzi Bubu’ analimudu vyema.
Muigizaji huyo pia amesema anashangaa kwanini Irene ameendelea kuongea sana kuhusu mpenzi wake wa zamani H.Baba wakati kila mmoja ana maisha mapya na mpenzi mpya.
Amesema hafurahishwi na tabia hiyo ya Irene ya kumsema na kumzushia scandal H.Baba ambaye huwa hapendi kuzungumza mambo hayo hadharani, tena kwenye vyombo vya habari.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents