Burudani
Flaviana Matata na Gado watajwa miongoni mwa Waafrika wenye ushawishi 2014
Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata na mchoraji mahiri wa vibonzo anayefanyia kazi nchini Kenya, Godfrey ‘Gado’ Mwampembwa, wametajwa na jarida la New Africa kwenye orodha ya mwaka 2014 ya Waafrika wenye ushawishi zaidi.
Flaviana ameungana na muigizaji wa Kenya, Lupita Nyong’o kwenye orodha hiyo yenye wanawake 40.
Thanks,I am humbled"@CNsekela: @iGaddo FlavianaMatata Congrats to our compatriots who are on the list of 100 Most Influential Africans!"
— Flaviana Matata (@FlavianaMatata) November 26, 2014
Hata hivyo Nigeria na Afrika Kusini ndizo zimetawala orodha hiyo zikiwa na watu 33 na 27.
Kwenye orodha hiyo pia kuna viongozi wanne wa nchini wakiwemo Rais Uhuru Kenyatta, Rais al-Sisi wa Misri, Rais Déby wa Chad na Museveni wa Uganda.