Bongo Movie
Filamu ya Aunt Ezekiel ‘Scola’ yapigwa stop kuingia sokoni kutokana na kwenda kivyume na maadili
Baada ya bodi ya filamu nchini miezi kadhaa iliyopita kuizua fimu ya Sister Mary ya Ray isiingie sokoni kutokana na kulichafua kanisa katoliki, Aunt Ezekiel naye yamemkuta.
Kwa mujibu wa Global Publishers, filamu yake iitwayo Scola imezuiwa kuingia sokoni kutokana na kuwa na sehemu zinazodaiwa kuwa kinyuma na maadili ya Kitanzania.
Imedaiwa kuwa filamu hiyo imegundulika kuwa na matatizo hayo baada ya muigizaji huyo kuipeleka kwenye bodi hiyo ili ikaguliwe kabla ya kuingia sokoni na sasa amepewa kazi ya kuondoa vipande hivyo ili ihakikiwe tena kwa mara nyingine.