Michezo

FIFA yaiondolea Nigeria marufuku iliyoiwekea mwezi huu

Shirikisho la soka duniani FIFA limeondoa marufuku lililoiwekea Nigeria isishiriki mashindano yoyote ya kimataifa.

Blatter1

Shirikisho hilo lilikuwa limeipiga marufuku Nigeria kutoshiriki katika michuano yoyote ya soka ya kimataifa mapema mwezi huu kwa kuwa serikali ya Nigeria iliingilia uongozi wa shirikisho hilo nchini Nigeria.

FIFA imeamua kuchukua uamuzi wa kuondoa marufuku hiyo baada ya mahakama kuondoa agizo la kuwatoa baadhi ya maafisa wakuu wa shirikisho hilo nchini Nigeria.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents