Michezo

FIFA kumlipa mshahara Coleman kwa kuvunjwa mguu

Shirikisho la soka duniani FIFA limethibitisha kuwa litamlipa mshahara beki wa timu ya Taifa ya Jamhuri ya Ireland na klabu ya Everton Seamus Coleman kwa kipindi chote atakachokuwa anauguza mguu wake.

Coleman alivunjika mguu wake wa kulia ijumaa iliyopita katika mechi dhidi ya Wales baada ya kuchezewa rafu mbaya na beki Neil Taylor, mechi hiyo iliisha kwa sare ya 0-0.

Siku ya jumamosi Coleman alifanikiwa kufanyiwa upasuaji na sasa anataraji kukaa nje ya uwanja kwa muda wa takribani miezi 6 akijiuguza.

FIFA kupitia (Fifa Club Protection Programme) wamethibitisha watakuwa wanamlipa mchezaji huyo kwa kipindi hicho chote atakachokuwa nje ya uwanja. Mshahara wake ambao kwa wiki ni Pauni 50,000.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents