Burudani
Fid Q hajawahi kusikiliza ngoma za Nash MC!!
Fareed Kubanda aka Fid Q alipata F kwenye somo la unafiki so mara nyingi hujitahidi kuwa mkweli vyovyote inavyowezekana.
Japo siku za hivi karibuni utaratibu wake wa kuruhusu maswali kutoka kwa mashabiki wake, AskFidQ umeonesha kutawaliwa na maswali yale yale, leo tumegundua something very interesting kwamba Ngosha hajawahi kumsikiliza Nash MC aka MC pekee mwenye VVU (Vina Vikali Usipime).
Hiyo ni baada ya shabiki mmoja aitwaye Innocent kumuuliza: Unaamini Nash Mc anasifa kamilifu za kuitwa MC? Fid amejibu: Honestly.. Sijawahi kumsikiliza so sina jibu la swali lako.