Burudani

Fid Q ampongeza Harmorapa, ataka wasanii wanaotaka ‘kukiki’ wauone uongozi wa rapper huyo

Msanii wa muziki wa hip hop kutoka Mwanza, Fareed Kubanda aka Fid Q amedai Harmorapa ni mmoja kati ya wasanii walioweza kufanya ‘shoo bizi’ na kufanikiwa.

Akiongea na Bongo5 wiki hii, Fid Q amedai kama kuna msanii anataka kufanya ‘shoo bize’ ni bora afanye kazi na uongozi wa rapper huyo.

“Harmorapa na management yake wamefanikiwa kucheza na kitu kinaitwa shoo bizi, watu wote sasa hivi wanamjua Harmorapa ni nani, ambacho amebakiza ni kutoa kazi ya kueleweka ili aweze kufanya biashara,” alisema Fid Q.

Aliongeza, “Kwahiyo kama kuna mtu anataka kujifunza shoo bizi unatakiwa kuwa chini ya management ya Harmorapa, watu watakufahamu haraka na kila kitu kitakuwa sawa,”

Rapper huyo alidai Harmorapa hakusema yupo level zake bali alisema akikuwa anataka kuwa level za akina Fid Q.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents