Burudani
Faiza Ally: Kama mwanamke ninatamani sana kuolewa
Msanii wa filamu na mwanamitindo mwenye vituko, Faiza Ally amesema angependa kuolewa lakini wanaume wengi si waoaji.
Faiza na mwanae Sasha
Faiza ambaye amezaa mtoto mmoja na mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph ‘Sugu’ Mbilinyi ameiambia Channel Ten kuwa kila mwanamke anatamani aolewe na awe na familia.
“Wachumba hakuna siku hizi wa kuoa,” alisema Faiza. “Hakuna mwanaume wa kuoa. Kila mwanamke ana ndoto ya kuolewa na kuwa na familia, mimi mmoja wapo na ndoto ya kuolewa lakini wanaume wenyewe wamekuwa magumashi. Siamini kama kuna mwanamke hataki kuolewa.”