Technology

Facebook nayo yaja na mtindo wa Snapchat

Baada ya Instagram kuanzisha Insta Stories, mtindo ulioipandisha chat Snapchat, Facebook nayo imekuja na mtindo huo kwenye app yake.

Kupitia app ya Facebook, sasa unaweza kushare matukio/stories na kuona kile marafiki zako wamekifanya kwa saa 24. Juu ya Facebook app, utaona picha za duara zinazowakilisha story walizoziweka marafiki zako na ukibonyeza, utaona picha, video ama michoro waliyoweka.

Baada ya saa 24, post hizo zitapotea na hazitaonekana tena.

Kwa maana hiyo Facebook sasa imeanzisha stories kwenye app zake zote, Facebook, Messenger, Instagram na Whatsapp. Hadi sasa Instagram stories zimekuwa na mafanikio makubwa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents