Exclusive Pics: Damu, Minyororo na Vinyago – Video ya ‘Mr Nay’ inatisha
Weka mbali na watoto, video ya ‘Mr Nay’ inatisha. Nay wa Mitego anayefahamika kwa kufanya mambo nje ya Kumi na Nane kama Weusi, yupo nchini Kenya ambako amekamilisha kushoot video ya ngoma yake mpya na muongozaji Kelvin Bosco Jr.
Mfalme Nay?
Katika picha ambazo Bongo5 imezipata exclusively kutoka Kenya, rapper huyo anaonekana kushoot video kwenye chumba kinachoonekana kama pamefanyika mauaji ya kimbari huku yeye akiwa amekaa kwenye kiti cha enzi kilichotapakaa damu. Kunaonekana jacuzzi lililojaa dimbwi la damu na wasichana waliofungwa minyororo kama watumwa wakicheza mbele yake.
Too cruel for TV?
Blood and Halloween costumes
Bosco Jr akiwa kazini
Show me what you got girl
Nay na waigizaji kwenye video hiyo wakionekana kusikiliza kwa makini maelekezo ya director
Akiwa Kenya, Nay wa Mitego ameimbia Bongo5 kuwa kuna uwezekano wa kufanya pia kolabo na Jaguar au DNA.
“Kenya nimekuja kushoot video yangu mpya Mr Nay chini ya director Kelvin Bosco Jnr na nimeshashoot nimemaliza. Kwahiyo sasa hivi ninavutavuta tu kwasababu nimekutana na watu wengi kwahiyo lolote linaweza kutokea,” Nay ameiambia Bongo5.
Stylist akiwa kazini kuhakikisha muonekano wa Nay unakuwa bomba
Tupo kwenye mipango ya kolabo panapo majaliwa kama sio leo, kesho tunaweza tukaingia studio kufanya kitu, lakini nafikiri mpaka baadaye tukionana nafikiri ndo tutapanga hiyo mipango zaidi kwa sababu tangu jana tupo pamoja tunapeana kampani kwenye location,jioni tunaenda studio so sijajua nini kitatokea. Kuna watu wawili kati ya Jaguar au DNA tunaweza tukafanya kitu,” amesema.
Nay akirap huku models walioshikiliwa utumwa wakicheza
Jacuzzi la damu: Model akichezea damu kwenye set ya video hiyo
Shika damu hizo: Models wakiwajibika
Maelekezo ya director: Sasa hapa inabidi ukaze, onesha ubandidu zaidi
King Nay: Niangalia vizuri machoni, unaona nini?
Ubandidu Ubandiduni
Red + White + Chains =?