Burudani

Barakah Da Prince amvisha Naj ‘Pete ya Ahadi’

Barakah Da Prince ambaye kwa sasa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii wa kike, Naj, amedai kupiga hatua zaidi kuelekea kwenye uchumba.

barakah_daprince

Wamefunguka exclusively kwa Bongo5 kuhusu uhusiano wao:

“Yeah ni kweli mimi na Naj tuna uhusino na hadi kwetu nimeshamtambulisha na yeye kwao najulikana na pia nimemvisha pia pete, sio ya uchumba ila ni Promise Ring,” amesema Barakah.

barakah-1-656x800

“Ndio hivyo yaani kuna kazi pia ambazo tumefanya ila hazitatoka sasa hivi hadi kwanza kila mtu atoe single yake halafu ndio itakuja hiyo ngoma ya pamoja mimi na Naj,” ameongeza.

baranaj 4

Kwa upande wake Naj amesema:

Ni kweli Barakah amenivisha pete kama alivyosema. Kwangu ni furaha sana maana nimeshakuwa na mahusiano yaliyopita lakini sikuwahi kufanya kitu kama hiki. Naona kabisa kuwa mahusino haya ni ya ukweli na naona kuna malengo kabisa, nafurahia kwakweli.”

“Bado hatujaanza kuishi wote ila muda mwingi tupo pamoja, nafurahia mahusiano yangu ya sasa. Ni kweli tumefanya ngoma ya pamoja lakini haitatoka sasa hivi mimi natakiwa niachie ngoma yangu na pia nishoot video, halafu pia nitarudi Uingereza mara moja, kuna vitu vyangu kule then nitarudi tena Bongo.”

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents