Michezo

Eto’o astaafu soka ya kimataifa akiwa na miaka 33

Mfungaji mabao mengi zaidi wa timu ya taifa ya Cameroon Samuel Eto’o ametangaza kustaafu soka ya kimataifa.

Samuel-Eto’o-–-Cameroon

Mshambuliaji huyo ambaye ameifungia Cameroon mabao 56 amejiunga na Everton ya Uingereza juzi .

Kufuatia kauli hiyo, Eto’o sasa hatakuwepo katika kipindi chote cha kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwezi Januari mwakani.

“Nataka kuwajuza kuwa nimestaafu mashindano yote ya kimataifa ”aliandika Etoo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram .

Mechi yake ya mwisho ilikuwa dhidi ya Mexico

“Ningependa kuwashukuru sana mashabiki wangu kote barani Afrika na duniani kwa mchango wao .”

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona, Inter na Real Madrid alicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa mwaka wa 1997 Cameroon iliponyeshewa 5-0 na Costa Rica.

Mechi yake ya mwisho ya kimataifa ilikuwa dhidi ya Mexico katika kombe la dunia huko Brazil.

Source:BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents