Habari

Esther Wassira awashutumu madaktari kwa kifo cha uzembe cha mtoto wa rafiki yake


Mwanamuziki wa zamani ambaye kwa sasa ni mwanasheria, Esther Wassira amewatupia shutuma nzito madaktari wa hospitali ya Amana ya jijini Dar es Salaam kwa kile alichokiita ‘uzembe’ wa makusudi uliosababisha kifo cha mtoto mchanga wa rafiki yake.
“Naenda pia kwenye msiba wa rafiki yangu amefiwa na mtoto wake wa siku moja,aliyefia hospitali Amana,baada ya Madaktari kuwachomolea watoto ishirini Oxygen na kuwaacha wakiteketea!!! Kweli jamani??? Doctors??? You can kill innocent infants??? Si mngewaachia hiyo oxygen tu mkaondoka??? Serikali!!! Do something jamani..! Just give them what they want!! Think of the loss..mama abebe mimba miezi tisa,mwanae auliwe?” Esther aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.
“This is a catastrophe to the nation..hivi kweli!!!!, it is very serious..yupo kwa mama yake anakandwa tumbo na mwanae ameshamzika!!! This is BAD! Naogopa nchi yangu!!”
Hata hivyo shutuma hizo nzito dhidi ya madaktari wa Amana zilizotolewa na mwanadada huyo zilipokelewa kwa hisia tofauti kutoka kwa watu wengine.
“Pole na msiba huo..ila usiwe unakurupuka na kuleta uzushi kuwa madaktari wamewachomolea oxygen watoto..ukiambiwa thibitisha sijui utasemaje…u r a lawyer..think before u leap….usiwe kama layperson kukurupuka na kusema habari za uvumi….madaktari sio wajinga kama serikali yako kufanya kitu kama hicho kwa infants kama hao….kifo cha watoto ni kawaida tu..kama ingekuwa hakuna huu mgomo na kukatokea hilo sidhani kama ungesema hivyo Esther,” aliandika mtu mmoja aitwaye Pedro Juan.
“Pedro usinifrustrate!! I have enough frustrations!!! Ninakwambia am sitting with a woman hapa my friend ananiambia exactly what has happened wewe unaniambia uzushi!!! Ni heri ushtuke na uombe kuliko kunistress zaidi..do you think I want to accuse doctors au unadhani nafurahi kuona insensitivity ya government!! Am a human being,a woman for that matter!! Lawyer or not!!!,” alijibu Esther.
Mtu mwingine aitwaye Isaac Ruge Abraham alisema, “Nimeisoma hii post na kusikitika sana.Mimi na daktari kwa miaka 6 sasa na siamini kabisa kama kuna daktari anaweza kuchomolea watoto oxygen kwa madai yake.Kama amefanya hivyo ni kosa la jinai.Ila kama kuna mgomo na daktari hakwenda wodini kwa sababu kuna mgomo haya ni mambo mawili tofauti.
Kwa sasa mgomo umekamata pabaya maana hakuna hata emergencies zinazoguswa na ni kipindi kibaya sana kuumwa hata kama wewe ni daktari.Nadhani ni vibaya kutumia maelezo ya upande mmoja na kuyatumia kuweka presumptive judgement.
Esther Wasira mdogo wangu.Kwa kazi hii madaktari hujitoa mara zote wanapofanya kazi wakati mwingine bila kulala hadi masaa 36 na sidhani mtu anayejitoa kiasi hicho anaweza kufanya jambo kama ulilolielezea hapo.Wapo wazembe kwenye hii fani lakini hakuna wa kutenda hivi na kama yupo basi hafai kufanya fani hii.”
Kwa upande wake Esther aliongeza kwa kusema, “Isaac I do understand you brother..na wewe kama daktari umejibu vyema tena very objectively!! As you say,ni ngumu kuamini kuna daktari angekuwa mnyama kiasi hiki..what this lady was narrating on the incident ya mwanae,anasema,it was chaotic, they were many of them,charged into the room and switched them off,as a sign of “no more service guys”..!
Mimi nili-panic sana asubuhi..huyu mtu msibani anasema “cause of death” ni mwanangu kutolewa oxygen wakati akiwa Amana anaendelea na matibabu!! So as u say,it might be a presumptive judgment based on the testimony of the mother,but am not pronouncing anybody guilty!! I said earlier,if it gets to the level where the issue has been taken to the hands of the law and the accused tried,the state will declare their status,whether innocent or guilty!! Take this as a charge sheet,that’s the accusation,kinywa cha Mtanzania aliyepoteza mtoto wake ndio kimenena hayo!! So treat me as a spokesperson right now!!”
Mgomo wa madaktari nchini unaendelea kuchukua sura mpya kila kukicha,ambapo juzi Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari nchini Dr. Stephen Ulimboka, alitekwa na watu wasiojulikana walimpiga kinyama. Kwa sasa bado amelazwa katika hospitali ya Muhimbili akiendelea kupewa matibabu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents