Editor’s Pick: Ni kweli Lupita Nyong’o ameuweka matatani uhusiano wa Brad Pitt na Angelina Jolie? (Audio)
ANGELINA Jolie na Brad Pitt wanaidaiwa kuingia kwenye mgogoro uliosababishwa na si mwingine, bali ni Mkenya aliyeiteka Hollywood kwa muda, Lupita Nyong’o.
Lupita Nyong’o
Brad, mwenye miaka 50, anaidaiwa kumzimia kiukweli msichana huyo mwenye ngozi nyeusi angavu aliyetajwa kuwania kipengele cha muigizaji msaidizi bora wa kike kwenye tuzo za Oscar kwa kuigiza kama “Patsey” kwenye filamu iliyotayarishwa na Brad Pitt, 12 Years a Slave.
Brad Pitt
Pitt aliweza kuficha kikohozi cha upendo kwa Lupita mbele ya mkewe Angelina Jolie kwa muda lakini hivi karibuni alishindwa kujizuia kuusifia uzuri wa Mkenya huyo wakati wa halfa la Producers Guild Awards iliyofanyika huko Beverly Hills, Jan. 19.
Sikiliza kipande hiki cha sauti kumsikia mhariri wa Bongo5 akielezea mambo yalivyo na mtazamo wake kuhusiana na tetesi hii.