Mtangazaji wa Clouds FM Loveness aka Diva jana aliongozana na baadhi ya wasanii wa THT waliokuwa wakitimiza miaka saba katika kituo cha Al Madina Children Home kilichopo Magomeni Tandale Uzuri maeneo ya Yemeni jijini Dar es Salaam kutoa misaada mbalimbali kusaidia watoto wanaoishi kwenye kituo hicho.
Hiyo ilikuwa ni awamu nyingine kwa mtangazaji huyo kutoa misaada katika mradi wake wa Diva Giving for Charity. Katika ziara hiyo Diva na ujumbe wake walipata chakula cha mchana kwa pamoja na watoto hao.