Burudani

Ditto: Kundi la Mtu Pori lilishapita, ila tumebaki kama ndugu

Hitmaker wa Moyo Sukuma Damu, Lameck Ditto amefunguka kuhusu mipango ya kulirudisha kundi la Watu Pori.

Akiongea na mtangazaji wa Maisha FM ya Dodoma, Silver Touch, muimbaji huyo amesema kuwa kwakuwa hilo limepita hakuna mipango kama hiyo tena japo bado wanashirikiana kwa ukaribu na Afande Sele na MC Koba.

“Afande Sele na Koba ninaishi nao kama familia sio kwasababu kundi halipo hatushirikiani mambo yote, tunashirikiana sana. Kuhusu kulirudisha kundi la Watu Pori nadhani hilo limeshapita kwahiyo tunaendelea na mambo mengine lakini hilo halivunji undugu na ushirikiano tuliokuwa nao siku zote,” amesema Ditto.

Ditto ameongeza kuwa tayari ameshafanya nyimbo moja na Afande Sele lakini bado haijatoka.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents