Burudani
Director wa Uingereza kutayarisha documentary ya Whitney Houston
Director kutoka nchini Uingereza, Kevin Macdonald anajiandaa kutayarisha documentary itakayomuelezea Whitney Houston aliyefariki mwaka 2012.
Kelvin Macdonald ambaye amewahi kuongoza kutengeneza filamu nyingi kama vile, Marley, Touching The Void na filamu iliyompatia umaarufu mkubwa duniani ‘The Last King Of Scotland’ na nyingine nyingi.
Macdonald amesema kuwa stori haitazungumzia maisha ya Houston ila itaelezea ni jinsi gani alivyokuwa na uwezo mkubwa kwenye muziki.
Houston alikuwa ni mmoja kati ya wasanii wenye vipaji vikubwa duniani na waliowahi kuweka rekodi ya kuuza copy milioni 200 za albumu yake na amewahi kushika namba moja kwenye chati 100 za Billboard kwa mara saba mfululizo, Houston alifariki akiwa na umri wa miaka 48.