Diamond, Vanessa Mdee na Ommy Dimpoz washinda tuzo za Afrimma
Diamond Platnumz ameibuka na ushindi mkubwa zaidi kwenye tuzo za Afrimma zilizofanyika Dallas, Marekani alfajiri ya leo kwa saa za Afrika Mashariki.
Diamond ameshinda jumla ya tuzo tatu ikiwemo ya msanii wa mwaka
Muimbaji huyo ameshinda tuzo tatu; Best Dance Video ya wimbo wake Nana, Best Male East Africa na Artiste Of The Year.
Diamond amepost picha hiyo juu kwenye Instagram na kuandika: Dah, I really don’t know What to say, … dha! hata sijui nizungumze nini… (Eeh Mungu baba tunakushkuru sana kwa kuzidi kuunyanyua na kuupa Thamani mziki wetu wa Afrika Mashariki…tafadhali endelea kutushika mkono, usituache.
“EA well represented at the #Afrimma2015 & The Best Winner of the night goes to @diamondplatnumz with 3 Awards!! Salute all EA,” ameandika mtangazaji wa Citizen TV/Radio Citizen, Willy M Tuva aliyekuwepo kwenye tuzo hizo.
Pia wimbo alioshirikishwa na kundi la Bracket, Alive umeshinda tuzo ya Best Inspirational Song.
Vanessa Mdee ameshinda tuzo ya Best Female East Africa.
“Asante Asante Sana. You believed in me. Thank you,” ameandika kwenye Instagram.
Naye Ommy Dimpoz ameshinda tuzo ya Best New Comer.
#Afrimma2015 Best New Artiste Africa ? @ommydimpoz live from Dallas, Texas courtesy of @RadioCitizenFM cc @MsetoEA pic.twitter.com/wXo4ZfKh38
— Mzazi Willy M. Tuva (@mzaziwillytuva) October 11, 2015
Washindi wengine ni pamoja na Godfather (Best Video Director), AKA (Best Male South Africa, Best Collabo), Yemi Alade (Best Female West Africa), Davido (Best Male West Africa), Wizkid (Video of the Year, Ojuelegba), Yuri (Best Male Central Africa).