Burudani

Diamond: Sitaki kabisa kushika simu ya Zari naogopa kuumia!

Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa yeye na mpenzi wake Zari ni watu ambao huwa hawapendi
kupekuliana simu simu zao ili kuepukana na matatizo yanayoweza kusababishwa na simu za mikononi.

zari na dai

Simu za mikononi huwa ni moja ya chanzo cha ugomvi kwa wapenzi wengi, na tumekuwa tukisikia story za couple nyingi kuingia kwenye matatizo kutokana tu na mmoja kukuta ujumbe au picha zenye utata kwenye simu ya mwenzie hata kama haimaanishi kuwa anamsaliti.

Diamond na Zari wote ni watu maarufu ambao wana mashabiki wa jinsia tofauti, hivyo kwa kutambua mazingira ya kazi zao wameona ni bora kuaminiana bila kupekuana kwenye simu zao.

Diamonnd n Zari-phone

“Hicho ni kitu cha kwanza ambacho siwezi kudiriki kabisa,” alijibu Diamond alipoulizwa na Millard Ayo kama huwa anashika simu ya Zari.

Diamond aliendelea kutoa sababu za kutoshika simu yake, “sidiriki kwasababu namjua ni binadamu , unajua sometimes ukizingatia na yeye (Zari) ni mtu maarufu so sometimes watu wengine wanakuwa wanamsumbua, anaweza kukutwa na vishawishi sometimes anaweza akamjibu mtu akaitikia tu poa, kwangu mimi kikanikwaza kwasababu nampenda kwahiyo ikaniumiza, kwahiyo sitaki kabisa kushika simu yake.”

Pamoja na kwamba yeye hashiki simu ya mpenzi wake, vipi kuhusu Zari kushika simu yake?

“ Simu yangu mi haina password naiachaga tu lakini nafikiri na yeye ni mtu wa dizain hizo ambaye hataki kabisa kudiriki kushika simu yangu, yaani simu zinaleta ugombanishi sana.”

Diamond pia aliwashauri watu wengine kutoshika simu za wapenzi wao ili kuepukana na matatizo yanayoweza kuepukika.

“Kwahiyo simshauri mtu kushika simu ya mpenzi wake, cha muhimu tu kuzingatia kama anakupenda anakujali anakuheshimu na umuone na hivyo vitu, lakini kwenye simu yake mwache afanye chochote anachojua yeye.” Alisema Diamond.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents