Burudani

Diamond, Harmonize, AY, DJ D-Ommy washinda tuzo ya AEAUSA

Diamond Platnumz, Harmonize, AY na DJ D-Ommy wa Clouds FM wameshinda tuzo ya African Entertainment Awards USA zilizotolewa usiku wa kuamkia Jumapili huko New Jersey, Marekani.

14676769_631293397053066_2374060988388343808_n

Diamond ameshinda kipengele cha Best Male Single na pia kuungana na AY kwenye Best Collabo (Zigo Remix).

Harmonize ameshinda tuzo ya Best New Artist huku D-Ommy akishinda tuzo ya Dj bora.

Katika kushukuru kwa tuzo hiyo, Harmonize ameandika kwenye Instagram:

Najivunia kuwa mtanzania navyenye wenye Tanzania yao wanavyo ni support katika nyanja tofauti sina chakuwalipa ila nitahakikisha nafanya kile mnacho kipenda Asante kwa kunipigia kura na kuifanikisha tuzo hii nyingine africa kutuwa Tanzania……???????????? pia team mzima #Wcb kwa kuhamasisha upigaji kura M/mungu awabariki sanaa……..!!! uongozi mzzimaa #WCB kwakuwa nami bega kwa bega kuniongeza Mama Chiiiiibu @kendrah_michael umekuwa ukishauri mambo mengi sanaaaa mama angu sina cha kukulipa and mama Harmo umekuwa ukiniombea sana……!!!! niishie hapo kwaleo ila amini kuwa nina furaha naamini kuwa hii ni hatua moja wapo…….???? #Raj ♡

Tuzo hizo zilizokuwa zikirushwa live kupitia Trace Urban, zimetolewa saa chache baada ya zile za MTV MAMA ambapo hakuna msanii wa Tanzania alishinda.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents