Burudani

Diamond au Alikiba? Mr Blue aeleza yupi anayependa kufanya naye ngoma

Kihistoria, Diamond na Alikiba ni wadogo zake Mr Blue. Wakati Mr Blue anatamba na ngoma zake ikiwemo Mapozi, hakuna aliyekuwa akiwafahau wawili hao.

IMG_7980

Na kuna wakati Blue aliwahi kusimulia namna alivyokerwa na tabia ya Diamond ya kutembea na ex wake akiwe Wema na Najma. Hata Hivyo rapper huyo wa Pesa, amesema anawakubali wote Alikiba na Diamond na wote ni washkaji.

“Unajua mie wale wote washkaji zangu nawala sina tatizo nao kwahiyo nipo tayari kufanya kazi na yeyote yule ambaye atakuwa tayari si unajua hii kazi na kazi mkishirikiana pamoja ndo inakuwa nzuri zaidi,” Blue ameiambia Bongo5.

Akizungumzia kuhusu video, rapper huyo amesema anatarajia kutoa video mbili kwa pamoja.”Nimeshaulizwa sana kuhusu natoa video lini. Jibu sasa lipo tayari kwa mashabiki wangu. Nitaachia video mbili hivi karibuni na hizo video nimefanya zote na Adam Juma. Video ya Pesa ipo tayari na namalizia kushoot video ya Mapenzi pia kwahiyo muda wowote nitaziachia.”

Kwa upande mwingine Kabasyer amesema kama akitaka kurudi shule basi atasomea tu muziki na utayarishaji.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents