Burudani

Diamond atajwa kuwania tuzo za IRAWMA, Marekani kupitia ‘Mdogo mdogo’, anachuana na Davido, Awilo Longomba na Bracket

Kwa mara nyingine Diamond Platnumz ametajwa kuwania tuzo nyingine za kimataifa nchini Marekani, ambapo safari hii wimbo wake wa ‘Mdogo mdogo’ wenye miezi miwili tangu utoke umemuwezesha kuingia kwenye tuzo za IRAWMA (International Reggae and World Music Awards).

Irawma

Wimbo wa ‘Mdogo mdogo’ wa Diamond umeingia kwenye tuzo hizo katika kipengele cha ‘Best African Song/Entertainer’. Kwa mara nyingine Diamond anapambana na Davido anayewania kipengele hicho kupitia wimbo wake ‘Aye’.

diamond31

tuzo

Nominees wengine wa Afrika katika kipengele hicho ni “Bundeke” – AwiloLongomba (Congo), “Mama Africa” – Bracket (Nigeria), “Tam Tam” – Willy Paul Msafi (Kenya), “Sitya Loss” – Eddy Kenzo (Uganda).

DABO
DABO

Diamond hataipeperusha bendera ya Tanzania peke yake, msanii wa dancehall DABO pia anawania kipengele cha ‘Best New Entertainer’.

Tuzo zitatolewa Jumamosi October 4, 2014 Coral Springs center For The Arts, Florida, Marekani.

Upigaji wa kura tayari umeanza kupitia www.irawma.com, ili kumpigia kura Diamond fuata link hii (http://irawma.com/irawma_vote2014), kisha tafuta kipengele cha ‘Best African Song/Entertainer’, na kumpigia kura DABO tafuta kipengele cha ‘Best New Entertainer’.

Kuhusu IRAWMA:

The mission of the International Reggae & World Music Awards (IRAWMA), established in 1982 acknowledges and honors the accomplishments and contributions of reggae and world music artists, including: songwriters, performers, promoters and musicians. Produced by Martin’s International & Associates, the IRAWMA has been staged in many major cities including: Atlanta, Chicago, Fort Lauderdale, Miami, New Orleans, New York as well as both Montego Bay and Ocho Rios Jamaica. The impetus behind the IRAWMA is it’s commitment to promoting greater participation and acceptance of Reggae, Caribbean and World Music, Internationally.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents