Burudani

Diamond amesharekodi collabo na msanii mkubwa wa Marekani, hutaamini ni yupi!

Diamond Platnumz is unstoppable! Ni muda mrefu sasa tumekuwa tukisikia tetesi kuwa amerekodi ngoma na msanii mkubwa wa Marekani japo hakuwahi kumtaja, lakini sasa tunaweza kuwa na ubashiri sahihi!

11032973_815690111830345_1382282765_n

Muimbaji huyo alikuwa akiongea kwenye kipindi cha 360 cha Clouds TV leo asubuhi ambapo aliulizwa ni msanii gani wa nje ya Afrika anayependa kufanya naye kazi.

Diamond alidai kuwa tayari msanii anayemkubali zaidi nchini Marekani ameshafanya naye kazi japo hakupenda kumtaja tena.

Aliombwa amtaje msanii mwingine tofauti na huyo na kusema wasanii watano anaowapenda zaidi nchini Marekani ni Nicki Minaj, Chris Brown na Usher Raymond na kwamba mmoja kati ya hao tayari ameshafanya naye ngoma!

So ubashiri wetu ni Usher!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents