Baada Jumamosi hii kufanya show katika ufunguzi wa kombe la AFCON 2017 nchini Gabon akishirikiana na wasanii wengine akiwemo Mohombi na Lumino, Diamond Platnumz ameiweka wazi timu ambayo yeye binafsi anaishabikia katika michuano hiyo.
Timu hiyo ni Uganda. Staa huyo ameziweka wazi sababu 2 zilizomfanya kuishabikia timu hiyo.
“Nitaishabikia Uganda, kwanza ni mashemeji zangu halafu ndio timu pekee iliyotoka East Africa,” alisema Diamond kwenye mahojiano na Sports Extra ya Clouds FM.