BurudaniDiamond Platnumz

Diamond afungua mwaka na deal hii kubwa ya ubalozi

Msanii wa muziki Nassib Abdul maarufu, Diamond Platnumz ameteuliwa rasmi na kampuni ya GSM kuwa balozi wa kutangaza bidhaa mbalimbali za taasisi hiyo.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa kampuni hiyo, Lauma Mohamed ameeleza kuwa Diamond
Platnumz ni msanii mkubwa sana ndani na nje ya Afrika, hivyo wanaimani atakuwa balozi mzuri kwa bidhaa zao
bora kwa watanzania.

Kwa upande wake Diamond Platnumz ameeleza kuwa anafarijika sana kuona wasanii watanzania wanapata nafasi
ya kuwa mabalozi, kwani wasanii ni wengi lakini yeye amepata heshima hiyo hivyo ana imani ni jambo jema kwa tasnia ya muziki.

Ameongeza kuwa hapo mwanzo bidhaa nyingi kwa mfano samani za ndani zilikuwa zinaagizwa nje ya nchi lakini kwa
sasa itakuwa rahisi kwani GSM kwenye duaka lao la ‘The New Home’ wanauza samani hizo halkadhalika nguo za watoto.

Licha ya kumtambulisha msanii huyo kama balozi mpya wa GSM wamezindua matangazo mapya mawili yaliyoigizwa na msanii
huyo pamoja na familia yake akiwemo Zari the Boss Lady na mtoto wao Tiffa, huku tangazo moja likiwa la nguo na lingine la samani za ndani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents