Burudani
D’Banj kuwadondosha Amber Rose na Blac Chyna Nigeria weekend hii
Staa wa Nigeria, D’Banj anatarajia kuwadondosha Amber Rose na Black Chyna nchini Nigeria kwenye event yake ‘10th Anniversary Movement’ itakayofanyika weekend hii Jan 31, 2015 jijini Lagos.
Amber Rose na Blac Chyna
Ex wa rapper Wiz Khalifa, Amber Rose ndiye atakuwa host wa shughuli hiyo. Kupitia Instagram Amber amethibitisha kwenda Naija kwa kuandika:
“Lagos, Nigeria I’m coming to Turn Up with my Friend D’banj January 31st for His 10th year Anniversary Weekend! #1 Kokolet @tmerritt234”.
Amber Rose ambaye amezaa na rapper Wiz Khalifa na Chyna aliyekuwa na uhusiano na rapper Tyga walianza kuwa karibu sana baada ya mahusiano na wapenzi wao kuvunjika mwaka jana 2014.