Burudani
D’banj apanga kufungua kesi dhidi ya kampuni ya simu
Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria, D’banj amepanga kuishtaki kampuni ya mtandao wa simu kwa kosa la kutumia kazi zake bila makubaliano.
D’Banj ambaye pia ni host wa kipindi cha Lip Sync Africa, kinachoruka kupitia kituo cha televisheni, MTV amepost ujumbe kwenye akaunti yake ya Instagram uliosomeka, “A certain telecom in Nigeria has been milking off my sweat illegally and I just caught them. This isn’t funny. I ‘ii take action soon.”
Hivi karibuni pia tumeshuhudia wasanii wa Bongo Fleva, AY na Mwana FA waliishtaki kampuni ya mtandao wa simu hapa ya Tanzania kwa kutumia kazi zao kinyume na sheria na kuamriwa kulipwa kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 2.