Burudani

Davido kushoot video mbili kwa mpigo wiki hii Marekani

Baada ya mastar wa Nigeria P-Square, Wizkid na Iyanya kuachia video zao mpya ambazo wote wameshoot Marekani hivi karibuni, hit maker wa ‘Aye’, Davido naye anatarajia kushoot video mbili kwa mpigo jijini New York, Marekani wiki hii.

Davido-600-x-450

Davido katumia facebook yake kuwatangazia dancers na warembo wa Marekani watakaopenda kushiriki kwenye video hiyo.

“Shooting 2 videos this week in NYC… Need amazing dancers,beautiful ladies for lead role & extras to come party with us… let’s ball and turn up for NEW YORK CITY one more time!…”

davido

Mwanzoni mwa mwezi huu (September) Davido ambaye ameshinda tuzo nyingi mwaka huu ikiwemo BET, aliachia single mpya aliyomshirikisha Dj Arafat iitwayo ‘Naughty’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents