Burudani
Davido analipwa shilingi milioni 146 za Tanzania kutumbuiza Kenya mwezi ujao!
Davido analipwa $80,000 (zaidi ya shilingi milioni 146 za Tanzania) kutumbuiza jijini Nairobi, Kenya mwezi ujao.
Mtandao wa Niaje wa Kenya umeandika kuwa staa huyo wa Nigeria anadondoshwa nchini humo na kampuni ya SkyHitz Global promoters.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Shaffie Lasie alisema bei hiyo pia ni baada ya kupunguziwa kidogo kwakuwa waliwahi kufanya kazi nyingine nchini Malaysia.