Burudani
Davido ampongeza Wizkid kwa kutoa album mpya
Davido amethibitisha kuwa hana kinyongo cha mafanikio ya msanii mwenzake Wizkid ambaye wiki kadhaa zilizopita wamekuwa wakirushiana vijembe kupitia Twitter, na baadae kila mmoja kukana kutokuwa na beef na mwenzie katika mahojiano waliyofanyiwa hivi karibuni kwa nyakati tofauti.
Davido ametumia akaunti yake ya Twitter kumpongeza Wizkid na P-Square ambao wameachia album zao mpya na kuwaombea Mungu awabariki.
Album mpya ya Wizkid inaitwa AYO na album mpya ya P-Square inaitwa DOUBLE TROUBLE.