Michezo
David Moyes akamata kazi ya kuinoa Real Sociedad
Kocha wa zamani wa Manchester, David Moyes ametajwa kuwa meneja mpya wa klabu ya Hispania, Real Sociedad.
Hiyo ya kwanza tangia atimuliwe kama meneja wa United mwezi April mwaka huu baada ya kufanya kazi kwa miezi 10. Moyes amechukua nafasi ya Jagoba Arrasate, aliyeachishwa kazi na Sociedad kutokana na kuwa na matokeo mabaya.
Raia huyo wa Scotland amesaini mkataba hadi June 2016 na kazi yake ya kwanza itakuwa dhidi ya Deportivo, tarehe 22 November.