David De Gea atwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi, Man United
Mashabiki wa club ya Manchester United walipiga kura za kumchangua mchezaji bora wa mwezi na asilimia 70 ya kura zote zilimchagua kipa namba moja wa klabu hiyo, David de Gea, 23, kama mchezaji bora wa mwezi katika kikosi hicho.
Baadhi ya mechi alizoakoa magori ya wazi na kumpa sifa kubwa Mhispania huyo ni pamoja na mechi dhidi ya West Brom, Everton na mechi ya Chelsea pale alipookoa michomo mingi ya wazi ikiwa ni pamoja na ule uliopigwa na Eden Hazard.
David de gea akiokoa shuti la Eden Hazard katika mchezo dhidi ya Chelsea ulioishia kwa sare ya 1-1 katika uwanja wa Old Trafford
Katika hatua nyingine, Manchester City itawakaribisha watani wao wa jadi Manchester United katika dimba la Etihad Jumapili ya tarehe 2 November.
kati ya mikwaju uliyookolewa na De Gea katika mechi dhidi ya Everton
Kikosi cha Man City kina weza kuwakosa wachazaji wake muhimu kama David Silva pamoja na Yaya Toure waliopata majeraha katika mechi ya kombe la FA dhidi ya Newcastle.