Burudani

Cyrill Kamikaze: Napigania kuachia albamu mwaka huu, ikishindikana nitauzia dukani kwangu

Rapper Cyrill Kamikaze amefunguka juu ya mpango wake wa kuachia albamu kama walivyofanya Navy Kenzo na baadhi ya wasanii walioahidi kufanya hivyo mwaka huu.

Akiongea katika kipindi cha Flavour Express cha Maisha FM, Silver Touchez, Rapper huyo amesema anapigania kuachia albamu mwaka huu japo kwenye swala la uuzaji ndio tatizo lakini ikishindikana atauzia hata dukani kwake.

“Mimi nini ngoma nyingi sana zipo studio. Actually nina ngoma nyingi mpaka nyingine zimekuwa outdated kwa sababu nimekuwa nikirekodi sana. Situation ya kutoa albamu Bongo imekuwa tatizo kidogo nikisema nitoe nitajuliza nitaanzia wapi kuiuza?,” amesema Cyrill.

“Lakini kuanzia mwaka jana, mwaka juzi ilikuwa ni ndoto yangu lakini kunakuwa na mambo mengi yanaingiliana. Lakini mwaka huu ninataka kupigania hili suala niwe na albamu mkononi na ikishindikana basi nitaiuza hata dukani kwangu,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents